JERUSALEM

Kwa nini mji wa Jerusalem ni mtakatifu?

Religious sites in Jerusalem's Old City
Kumekuwa na mzozo wa muda mrefu kuhusu udhibiti wa mji wa Jerusalem kati ya Waisraeli na Wapalestina.
Mji huo kwa sasa huwa umegawanywa mara mbili, Jerusalem Mashariki na Jerusalem Magharibi.
Jerusalem ya Magharibi hutazamwa na Israel kama mji wake mkuu nayo Jerusalem Mashariki hutazamwa kuwa mji mkuu wa taifa la Wapalestina (litakapoundwa), ingawa eneo hilo bado kwa kiwango kikubwa limetawaliwa na Israel tangu vita vya 1967.
Tangu wakati wa vita hivyo, Israel imejengwa nyumba za walowezi wa Kiyahudi takriban 200,000 ambao huishi Jerusalem Mashariki, hatua iliyoshutumiwa na jamii ya kimataifa. Eneo hilo huishi Wapalestina takriban 370,000.
Israel ilitangaza 1980 Jerusalem yote kuwa mji wake mkuu wa milele, lakini nchi nyingi duniani hazikubali azimio hilo.
Hivyo basi, balozi za nchi za kigeni katika Israel ziko nje ya Jerusalem, katika mji wa Tel Aviv.
Mzozo huo umefufuliwa tena kutokana na hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani kutarajiwa kuutambua mji huo kama mji mkuu wa Israel.
Mataifa mengi ya Kiarabu yameshutumu hatua hiyo ya Bw Trump na kusema itazidisha uhasama Mashariki ya Kati.
Lakini ni kwa nini mji huu huzozaniwa hivyo? Mwandishi wa BBC Erica Chernofsky anachambua.

Dini tatu

Mji huu huwa na umuhimu mkubwa kwa dini tatu kuu - Ukristo, Uislamu na Uyahudi. Dini zote tatu humuangazia Abraham anayetajwa kwenye Biblia na Koran kama mmoja wa waanzilishi au mababu wa imani.
Ni mji ambao umedhibitiwa na dini hizo kwa vipindi mbalimbali katika historia.
Kwa Kiebrania, mji wa Jerusalem hufahamika kama Yerushalayim na kwa Kiarabu al-Quds. Kwa Kiswahili, jina lake halisi ni Yerusalemu. Mji huo ni miongoni mwa miji ya kale zaidi ambayo ipo hadi sasa duniani.
Ni mji ambao umetekwa, ukabomolewa na kuharibiwa na kisha kujengwa tena.
Kila sehemu ya ardhi yake ukichimba kwenda chini hufichua enzi fulani katika historia yake.
Ingawa umekuwa chanzo cha ubishi na mzozano kati ya dini mbalimbali, dini zote huungana kwa pamoja kuungama kwamba ni eneo takatifu.
Ndani yake kuna Mji Mkongwe, ambao una njia nyembamba, vichochoro na nyumba za kale. Kuna maeneo manne makuu na kila eneo, majengo huwa tofauti. Kuna eneo la Wakristo, Waislamu, Wayahudi na Waarmenia. Eneo hilo huzungukwa na ukuta mkubwa wa mawe. Hapo, kunapatikana baadhi ya maeneo yanayoaminika kuwa matakatifu zaidi duniani.
Kila eneo kati ya maeneo hayo manne (unaweza kuyaita mitaa) huishi watu wa aina moja. Wakristo wana maeneo mawili, kwa sababu Waarmenia pia ni Wakristo. Eneo lililotengewa Waarmenia, ambalo ndilo ndogo zaidi kati ya hao manne, lina vituo vya kale zaidi vya Waarmenia duniani.
Jamii ya Waarmenia imehifadhi utamaduni wake wa kipekee ndani ya Kanisa la St James na nyumba kubwa ya utawala. Maeneo hayo mawili yamechukua sehemu kubwa ya mtaa huo wa Waarmenia.

Kanisa

Ndani ya mtaa wa Wakristo, kuna Kanisa Kuu la Kaburi na Ufufuo wa Yesu Kristo, ambalo ni muhimu sana kwa Wakristo kote duniani.
Hupatikana katika eneo ambalo lina umuhimu mkubwa katika kisa cha kusulubiwa, kufariki na kufufuka kwa Yesu.
Kwa mujibu wa utamaduni wa Kikristo, Yesu alisulubiwa hapo, katika Golgotha, au mlima wa Calvary. Kaburi lake linapatikana ndani ya kanisa hilo la kaburi na inaaminika kwamba hapo ndipo alipofufuka.
Kanisa hilo husimamiwa kwa pamoja na madhehebu mbalimbali ya Kikristo.
Sana huwa ni wahudumu wa kanisa la Kiothodoksi la Ugiriki, watawawa na mapadri wa Francisca kutoka Kanisa Katoliki la Roma na wengine kutoka kanisa la Waarmenia.
Kuna pia wahuudmu kutoka kanisa la Waothodoksi kutoka Ethiopia, Coptic na Syria.
Ni eneo ambalo mamilioni ya mahujaji wa Kikristo husafiri kila mwaka kwenda kuliona kaburi wazi la Yesu na kutafuta ufunuo na kuomba katika eneo hilo.
line break

Msikiti

Mtaa wa Waislamu ndio mkubwa zaidi kati ya maeneo hayo manne na ndani yake kunapatikana madhabahu ya Dome of Rock (Kuba ya Mwamba) na Msikiti wa al-Aqsa kwenye eneo linalofahamika na Waislamu kama Haram al-Sharif, au Mahali/Hekalu Patakatifu.
Msikiti huo ndio eneo la tatu kwa utakatifu katika dini ya Kiislamu na husimamiwa na wakfu wa Kiislamu ambao hufahamika kwa Kiarabu kama Waqf.
Waislamu huamini kwamba Mtume Muhammad alisafiri kutoka hapo hadi Mecca usiku na aliomba pamoja na roho za manabii wengine wote. Hatua chache kutoka hapo kunapatikana Dome of the Rock (Kuba ya Mwamba) ambapo kuna jiwe la msingi. Waislamu huamini kwamba ni kutoka hapo ambapo Mtume Muhammad alipaa mbinguni.
Waislamu hutembelea eneo hilo takatifu kila wakati katika mwaka, lakini kila Ijumaa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, mamia ya malelfu ya Waislamu hufika kuomba kwenye msikiti huo.
line break

Ukuta

Katika mtaa wa Wayahudi, kunapatikana Kotel, au Ukuta wa Magharibi ambao ni masalio ya ukuta wa nje uliozunguka lililokuwa Hekalu Takatifu.
Ndani ya hetalu hilo kulikuwa na Patakatifu pa Patakatifu, eneo takatifu zaidi katika dini ya Kiyahudi.
Wayahudi huamini kwamba hapo ndipo kulikuwa na jiwe la msingi ambapo kutoka kwake dunia iliumbwa.
Kadhalika, wanaamini ni hapo ambapo Abraham alikuwa amejiandaa kumtoa kafara mwanawe Isaac. Wayahudi wengi huamini kwamba Dome of the Rock ndipo lilipokuwa eneo takatifu zaidi ndani ya hekalu lililofahamika kama Patakatifu pa Patakatifu.
Leo hii, Ukuta wa Magharibi ndilo eneo la karibu zaidi ambalo Wayahudi wanaweza kufanya maombi yao.
Husimamiwa na Rabbi wa Ukuta wa Magharibi na kila mwaka hutembelewa na mamilioni ya mahujaji.
Wayahudi kutoka kila pembe ya dunia hutembelea eneo hilo kuomba na kukumbuka utamaduni wao, hasa nyakati za siku kuu za kidini.
Ukuta huo pia hufahamika kama Ukuta wa Maombolezo.
Je unatumiaje mitandao ya kijamii kukuingizia kipato?
Kwa ufupi, nguvu na umuhimu wa vyombo vya habari rasmi inazidi kupungua kila uchao kadri teknolojia ya mawasiliano inavyozidi kukua na kusambaa katika maeneo yote.

Image result for how do we use computers to earn money
Zamani, enzi zile za Rais Julius Nyerere na baadaye Ali Hassan Mwinyi, vyombo vya habari vilikuwa ni kila kitu. Hakukuwa na njia nyingine rahisi ya kufikisha ujumbe kwa watu, kinyume na vyombo hivyo.
Wakati wa Nyerere, si ilikuwa si tu vyombo vya habari, bali ilikuwa vyombo vya Serikali, hususan magazeti na redio. Usipopewa nafasi enzi hizo, kelele zako zitaishia huko mtaani. Labda utengeneze vipeperushi na isingekuwa kirahisi kihivyo.
Wakati wa Mwinyi, tulianza kuona mabadiliko ya sera yaliyoruhusu vyombo binafsi, redio, magazeti. Vituo vya televisheni navyo vikaja. Nazungumzia Bara. Mabadiliko haya yaliwapa watu uwezo zaidi wa watu wenye fikra na mawazo mbadala kupata fursa ya kusikika kuliko zamani, lakini bado vyombo vya habari vilikuwa ni njia pekee ya kufikisha ujumbe kwa watu.
Ni katika kipindi cha awamu ya tatu ya Benjamin Mkapa, mapinduzi ya vyombo vya kijamii huko duniani ndiyo yalianza kwa kufunguliwa tovuti iliyoitwa Six Degrees mwaka 1997, iliyowezesha watu kuweka wasifu wao na kukutana na marafiki.
Baada ya hapo, zikaanza blogu mwaka 1999. Hata hivyo, historia ya blogu Tanzania inaanzia mwaka 2004 pale mwanasheria na mwandishi wa habari Ndesanjo Macha alipoanzisha blogu ‘Jikomboe’ inayoaminika kuwa ndiyo ya kwanza ya Kiswahili.
Zilianzishwa blogu kadhaa kama Kisima cha Fikra na nyinezo. Sekta ya blogu ilipata nguvu kubwa na umaarufu mwaka 2005 (mwanzo wa utawala wa Kikwete) pale Issa Michuzi alipoanzisha blogu ya picha. Kwa maendeleo yaliyofikiwa sasa, blogu ni mtandao wa kijamii ambao ni ‘mhenga’. Hizi ni enzi za Instagram, Twitter, Facebook, Snapchat, Youtube nk.
Mabadiliko enzi za mtandao
Ukilinganisha na enzi zile, kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya habari. Kwa sasa, vyombo vya habari vya kijamii naweza kusema vinashindana na vyombo vikuu vya kizamani vya habari, redio, magazeti na televisheni. Huu ndiyo ukweli.
Siku hizi, haiwezekani kumnyima mtu nafasi ya kutoa ujumbe na mawazo yake kwa wanajamii, shukrani ziende kwa mitandao ya kijamii.
Hivi majuzi, Spika wa Bunge, Job Ndugai alikuwa anahangaika kupambana na wabunge wanaotoa matamko mitandaoni wakimkosoa.
Zamani ingekuwa rahisi. Unawanyima tu nafasi ya kuongea kwa kutoa maagizo au vitisho kwa vyombo vya habari. Akinyimwa jukwaa la kuongelea, angeishia kupiga kelele mtaani kwake. Hakuna ambaye angemsikia.
Hayo hayawezekani dunia ya leo kwani mitandao ya kijamii inampa kila mtu nafasi ya kusema, apendavyo. Ukikataliwa na vyombo vikuu, huna haja hata ya kumuomba mtu. Unafungua akaunti na kubwabwaja utakavyo.
Ukuu wa kurasa maarufu
Ukweli mpya ni kuwa watu maarufu wana ufuasi mkubwa, wanasomwa kuliko vyombo vingi vya habari.
Tafiti mbalimbali zinaonyesha kwa ujumla, vyombo vya habari yaani redio, televisheni na magazeti vimepoteza mapato ya matangazo kwa mitandao ya kijamii. Inawezekana kuna baadhi ya nchi, au vyombo fulani katika nchi husika, ambavyo vinafanya vizuri, lakini ukweli wa jumla ndio huo.
Mtangazaji akitaka kutangaza bidhaa yake iwafikie watu ataenda katika kurasa za watu maarufu, zenye wafuasi kwa mamilioni, hususan wasanii ambao kupitia wao unaweza kufikia watu wengi kuliko magazeti au redio nyingi ambayo labda husomwa au husikilizwa na mamia au maelfu.
Faida pekee ambayo vyombo vikuu inayo ni hadhi na heshima.
Kwamba mitandao ya jamii kwa ujumla wake inaonekana imejaa uongo, uhuni, matusi, kurasa feki, watu wasiojulikana nk. Faida nyingine kwa redio pekee ni kuwa ni bure kusikiliza, huhitaji MB na inafikia hata wasiojua kusoma na watu wa vijijini.
Mitandao ya kijamii imekuwa ikizalisha habari kubwa zinazotawala kurasa za mbele za magazeti, mara nyingi.
Wanasiasa wakubwa na machachari, siku hata hawana haja ya kuitisha mikutano ya habari. Wanaandika mawazo yao katika kurasa zao, na waandishi huchukua. Haya ni mapinduzi makubwa.
Mitandao ya kijamii imekuwa muhimu sana kiasi kwamba unaweza usiangalie habari siku nzima, lakini usipitwe na kitu iwapo upo kwenye mitandao.
Siku hizi hata habari za vituo vingi hurushwa mbashara katika mitandao ya kijamii.
Binafsi nikiwa ofisini, kama kuna tukio kubwa linaendelea na linarushwa moja kwa moja, basi nitaliangalia kupitia mitandao ya kijamii. Nakumbuka hata taarifa zote mbili za makinikia niliziangalia kupitia YouTube.
Mitandao ya kijamii inatupatia fursa kubwa ya kufikia maendeleo kiuchumi, kisiasa na kijamii. Kiuchumi, mitandao imeajiri watu wengi. Hivi sasa, shukrani kwa teknolojia hii, mamia ya watu wanapata mkate wao wa kila siku. Tusingekuwa tunazungumzia kampuni ya habari ya Millard Ayo na nyingine nyingi, bila mitandao, achilia mbali mamilioni ya pesa yanayoingia kwa watu kupitia matangazo.
Mitandao ya kijamii imerahisisha maisha ya watu. Kwa sasa, ni rahisi kupata taarifa za upatikanaji wa huduma mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii. Haja ya kusafiri ili kufanya biashara imepungua kwa hiyo mitandao pia imeokoa muda wa kusafiri.
Ubaya wa mitandao
Hivi majuzi nilikuwa katika ofisi ya ardhi pale Magomeni nikakutana na mzee mmoja wa zaidi ya miaka 60 wakati tukisubiri huduma. Katika mazungumzo, mzee alianza kutupia lawama mitandao ya kijamii kuwa haina faida yoyote zaidi ya kuharibu maadili na kuchafua jamii.
Wakati mzee anazungumza hayo, nilikuwa katika kundi la WhatsApp nikiendelea na majadiliano na waandishi wenzangu wa gazeti moja la wiki ninalolifanyia kazi muda wa ziada. Bila teknolojia hii, tungelazimika kukutana ana kwa ana kujadili mambo yetu. Ingekuwa ni kupoteza muda. Nikawaza mzee huyu ni katika watu waliokataa kubadilika kutokana na wakati. Amekwama katika zama za Nyerere. Ni bahati mbaya sana.
Hata hivyo, malalamiko ya mzee wangu yule si ya kupuuza moja kwa moja hata kidogo, ingawa suluhu si kuikataa teknolojia hii iliyoleta mapinduzi makubwa, bali kudhibiti matumizi yake, hususan katika ngazi ya mtu binafsi na kazini. Katika malalamiko yake, mzee alisema watu wanachati maofisini badala ya kufanya kazi, jambo ambalo ni la kweli kabisa. Pia, mzee alilalamika kuwa watu hutumia mitandao kuangalia na kutumiana picha za matusi. Pia, ni kweli. Zaidi ya hapo, alisema watu wamekuwa kama machizi, ambapo si ajabu kukuta wanacheka cheka hivyo, huku wakibofya bofya simu zao. Hii nayo ni kweli, ingawa sina hakika kama ni jambo baya.
Mitandao ina faida nyingi nilizozitaja tayari, lakini pia ina athari zake kubwa. Natamani tungeweza kudhibiti athari hizo ili mitandao isiwe sababu ya kurudisha nyuma maendeleo yetu. Kama alivyosema mzee, maeneo ya kazi, mfanyakazi yafaa asiruhusiwe kabisa kuingia na simu, lakini hii pia inategemea aina ya kazi.
Nchi nyingine na baadhi ya maofisi hapahapa Dar es Salaam, hususan katika balozi na taasisi za kimataifa, zinafanya hivyo. Watu wasiruhusiwe kuingia maofisini na simu, isipokuwa wale ambao kazi zao zinahitaji matumizi ya simu. Na hata hao, zitumike za ofisi.
Watanzania tunapenda umbeya na kufuatilia maisha ya watu wetu maarufu. Hivi majuzi mwanamuziki Diamond alipojitokeza katika redio kukiri kuwa amechepuka, mitandao ya kijamii ilichangamka. Watu walishinda huko kuangalia Zari kajibu nini, Hamisa anasemaje, Mange naye ametoa maoni gani na kufuatilia mijadala mbalimbali. Achilia mbali waliotoa maoni, kuna maelfu wanaosoma tu mijadala. Kazi zilifanyika sawasawa kweli?
Hawa wanaokesha mitandaoni ndiyo watumishi wetu wa umma na katika maofisi binafsi. Hawa ndiyo wenye uwezo wa kununua au kupata bure MB na hawa ndiyo wenye maarifa ya kutumia mitandao. Ni muda muafaka sasa, tudhibiti hili.
Mitandao ya kijamii ni jukwaa la mijadala, lakini mijadala yenyewe inayoongoza ikiwa ni kuhusu maisha ya watu, sina hakika kama tutafaidika sana.
Mitandao ya kijamii inapoteza muda wetu mwingi kwa sababu ina uraibu wa ajabu. Ukifungua ukurasa huu mara umehamia hapa, ukishtuka saa nzima imekwenda ukisoma posti za Wolper na Harmonize, Jux na Vanessa, Hamisa na Zaari wakirushiana madongo.

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

  • ()
Powered by Blogger.

Yaliyojiri leo

Tanzania yaanza majaribio dawa kinga ya Ukimwi

LIKE OUR FACEBOOK PAGE

Contact us

Name

Email *

Message *