NCHINI HISPANIA MAMBO YAMEKUWA MOTO

Catalonia kutangaza uhuru 'siku chache zijazo'

Catalonia itatangaza uhuru wake kutoka Uhispania siku chache zinazokuja, kiongozi wa eneo hilo amezungumza.

Katika mazungumzo yake ya awali tangu ifanyike kura ya maoni siku ya Jumapili, Carles Puigdemont alisema kuwa serikali yake itachukua hatua mwishoni mwa wiki hii au mwanzoni mwa wiki ijayo.

Kwa upande wake mfalme wa Uhispania Felipe VI, amasema kuwa waandalizi wa kura hiyo walikiuka sheria.

Vilevile amasema kuwa hali ya sasa nchini Uhispania sio nzuri na kutaka kuwepo umoja.

Maelfu ya watu kote eneo la Catalonia wamekuwa wakigoma kupinga ghasa za polisi wa Uhispania wakati wa kura, ambapo takriban watu 900 walijeruhwia.
Image result for catalonia people strike  pictures
Alipoulizwa Carles Puigdemont kuhusu ni kipi atakifanya ikiwa serikali ya Uhispania itaingilia kati na kuchukua udhibiti wa serikali ya Catalonia, Bw Puigdemont alisema kuwa yatakuwa ni makosa ambayo yatabadilisha kila kitu.

Bwana Puigdemont alisema kuwa sasa hakuna mawasiliano kati ya serikali mjini Madrrid na utawala wake.

Alipinga taarifa ya tume ya ulaya ya siku ya Jumatatu kuwa kile kinachoendelea Catalonia ni masuala ya ndania ya Uhispania.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

  • ()
Powered by Blogger.

Yaliyojiri leo

Tanzania yaanza majaribio dawa kinga ya Ukimwi

LIKE OUR FACEBOOK PAGE

Contact us

Name

Email *

Message *