Dkt. Shika kuiaga Tanzania mazima

Dkt. Louis Shika ambaye amejipatia umaarufu baada ya kutangaza dau la kununua nyumba za Lugumi, amesema kwamba hivi karibuni anatarajia kwenda kusihi Marekani, baada ya Umoja wa Mataifa kumpandisha cheo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Weekend Breakfast cha East Africa Radio, Dkt. Shika amesema awali alikuwa anafanya kazi kwenye shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi (UNHCR) na sasa amepandishwa cheo, hivyo hata ofisi zake hazitakuwa tena Nairobi nchini Kenya, kwani zitahamishiwa New York Marekani.
"Sasa hivi nina mpango wa kusajili kampuni yangu alafu mimi nisepe, nikiwa hapa nchini nanyanyasika, nilikuwa nafanya kazi na Umoja wa Mataifa  Bara la Afrika, sasa ni world wide ofisi itakuwa New York, nimepandishwa cheo, nafaya kazi ofisi ya UNHCR, hata mama Kevela alipogundua mimi ni balozi akasema nyinyi ndio mnaoongoza nchi hii, na watu wajue kuwa uteuzi wangu haukutokea Tanzania, nimeteuliwa kwa veto power, veto power ziko tano kwenye umoja wa mataifa, jina langu lilikuwa projected na Urusi na mwenyewe Putin", amesema Dkt. Shika.
Dkt. Shika ameendelea kwa kusema kwamba kura ambazo alipata zilitosha kwa yeye kuwa balozi wa Umoja wa Mataifa, kwani nchi tatu zilikubali jina lake kupitishwa ikiwemo na Marekani.
Share:

Download hapa majina ya walimu waliopangiwa vituo vya kazi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ametangaza ajira mpya 3,033 za walimu wa shule mbalimbali nchini za msingi na Sekondari ambao watakwenda kujaza nafasi za walimu waliobainika kuwa na vyeti feki.
Image result for selemani jafo kutangaza ajira mpya za walimu
Jafo alisema kuwa majina ya walimu hao wapya 3,033 yatatangazwa leo na kupangiwa vituo vya kazi, walimu 266 watakuwa ni walimu wa shule za sekondari na Walimu 2,767 watakuwa walimu wa shule ya msingi.
Aidha Jafo amewataka walimu hao wapya ambao wamechaguliwa kuripoti kwa Wakurugenzi wa halmshauri husika ambazo watakuwa wamepangia kuanzia Disemba 27, 2018 hadi Januari 7, 2018. 
Mbali na hilo Selemani Jafo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri ambazio walimu hao wataripoti kuwapokea na kuzingatia taratibu na kanuni zote za utumishi wa Umma na baadaye kutoa taarifa ya kuripoti kwao.
Orodha ya Majina ya walimu waliopangiwa vituo.pdf  DOWNLOAD
Share:

Tazama Ratiba ya 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya(UEFA)

Champions League draw: Chelsea face Barcelona, Tottenham to play Juventus

Image result for uefa icon
Chelsea have been drawn against Barcelona in the last 16 of the Champions League, while Tottenham will face Italian champions Juventus.
Premier League leaders Manchester City will play Switzerland's Basel, Manchester United face La Liga side Sevilla and Liverpool take on Portugal's Porto.
Holders Real Madrid will face Paris St-Germain.
A record five English teams progressed from the group stage this season.
Chelsea were the only English team to make it through as runners-up, with the other four sides all topping their respective groups.
The Blues have arguably been handed the most difficult tie, and it comes days after boss Antonio Conte conceded that their Premier League title defence was over following their defeat by West Ham, which left them 14 points adrift of Manchester City.
However, Chelsea did beat Barcelona in the semi-finals before lifting the Champions League trophy in 2012.
Real Madrid, who are aiming for a 13th title and third in a row, were given a tough draw against big-spending PSG after finishing behind Tottenham in Group H.
The group winners will be away in the round of 16 first legs on 13/14 and 20/21 February, and at home in the return matches on 6/7 and 13/14 March.
The final will take place in Kiev on 26 May.

Champions League last-16 draw

Juventus v Tottenham (13 February and 7 March)
Basel v Manchester City (13 February and 7 March)
Porto v Liverpool (14 February and 6 March)
Sevilla v Manchester United (21 February and 13 March)
Real Madrid v PSG (14 February and 6 March)
Shakhtar Donetsk v Roma (21 February and 13 March)
Chelsea v Barcelona (20 February and 14 March)
Bayern Munich v Besiktas (20 February and 14 March)
Share:

Ronaldo amtangazia vita Lionel Mess

  • Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amefikisha tuzo tano sawa na mpinzani wake Lionel Messi.

Cristiano Ronaldo amesema ataendeleza ‘vita’ na mpinzani wake mkubwa Lionel Messi katika mbio za kuwania tuzo za mchezaji bora wa dunia.

Ronaldo alitoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora akimshinda Messi. Mshambuliaji huyo wa Real Madrid imefikisha tuzo tano sawa na mpinzani wake.

Nafasi ya tatu ilichukuliwa na mshambuliaji wa Paris Saint Germain (PSG) Neymar. Tuzo hizo zinatolewa Ufaransa na kura zinapigwa na waandishi wa habari 173.

“Nitapambana naye (Messi), nitahakikisha nakuwa kwenye kiwango bora. Nitacheza vizuri kwa klabu na timu ya taifa,” alisema Ronaldo alipoulizwa kuhusu nafasi ya Messi.

Alisema ataendelea kulinda kipaji chake kwa manufaa ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno kwa kucheza kwa kiwango bora.

“ Nina furaha. Hili ni tukio kubwa katika maisha yangu, napenda kutoa shukurani kwa wachezaji wenzangu wa Real Madrid, pia nawashukuru watu wote walionifikisha hapa,” alisema Ronaldo.

Wakati wa kutoa shukurani, Ronaldo alitania anataka kupata watoto saba. Nguli huyo ana watoto wanne aliozaa na wanawake watatu tofauti.

Nyota huyo alikwenda Paris na ndege binafsi akiongozana na familia yake.
Share:

Polisi, TCRA wazungumzia akaunti ya Mange Kimambi

Jeshi la Polisi limetaka liachwe liendelee kufanya kazi yake kwa weledi katika kushughulikia suala la Mtanzania aishiye ughaibuni, Mange Kimambi, ambaye anatuhumiwa kuchapisha taarifa zinazodaiwa kuwatusi mitandaoni watu mbalimbali wakiwamo viongozi.


 Akizungumza na Nipashe  kuhusiana na uwezekano wa wao kuifunga akaunti ya Kimambi ikiwa sehemu ya hatua wanazochukua kwa sasa, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa, alisema ni kweli jeshi lao linalifanyia kazi suala hilo.
Hata hivyo Mwakalukwa hakutaka kukubali au kukataa juu ya kile kilichodaiwa kutokea kwenye akaunti ya Kikambi na badala yake kutaka apewe muda wa kulifanyia kazi ndipo alitolee maelezo ya kina.
Hili jambo lina mambo mengi sana. Watu wengi wanahusika na taasisi nyingi (pia) zitahusika kulishughulikia, Hivyo tunaendelea kupokea mawazo ya watu mbalimbali kuhusu namna ya kwenda nalo… mawazo wanayotupa tunayafanyia kazi lakini naomba mtuache kwanza tunaendelea kulishughulikia,” alisema Mwakalukwa.
Aidha wakati Msemaji wa Polisi akisema hayo, TCRA ilisema kuwa haiwezi kufunga wala kuingilia akaunti ya Kimambi kwa sababu huo siyo wajibu wake kisheria.
Msemaji wa TCRA, Semu Mwakyanjala, aliiambia Nipashe kuwa mamlaka yao haina nguvu za kisheria kufanya kazi hiyo bali wenye wajibu wa kufanya hivyo ni kitengo cha kudhibiti uhalifu wa mitandaoni cha Jeshi la Polisi.
Akifafanua zaidi, msemaji huyo alisema makosa yote yanayohusu mitandao, yakiwamo ya watu kutishiwa maisha, kutukanwa, kuibiwa kwa njia ya mtandao au kunyanyaswa kwa namna yoyote mtandaoni, wanaohusika ni polisi na siyo TCRA. 
Masuala ya akaunti za watu kwenye mitandao kama hiyo unayosema (ya Kimambi)… mwenye mamlaka ya kuingia na kuzifunga ni Jeshi la Polisi. Bunge liliipa mamlaka ya kisheria polisi kuchunguza na kukamata wahalifu kama hao… waulizeni wao,” alisema Mwakyanjala.
Hata hivyo zipo taarifa mitandaoni  zilimkariri Mtanzania huyo aishiye Marekani kuwa kilichotokea ni matokeo ya kazi ya wadukuzi wa mitandaoni, maarufu kama ‘hackers’ kupoteza akaunti yake yenye wafuasi takribani milioni 1.5.
Pamoja na hayo upo ujumbe wa lugha ya kigeni uliokuwa ukisambaa kwenye mtandao wa instagram ukionyesha kuwa akaunti inayofahamika kuwa ni ya Kimambi, imefungwa na waendeshaji wa mtandao wa Instagram kwa sababu ya kuwapo kwa malalamiko dhidi ya machapisho ya akaunti hiyo.
Share:

Wema sepetu karudi CCM

[​IMG]Wema Sepetu: Siwezi Kuendelea kuishi kwenye Nyumba inayo nikosesha amani... Peace of mind is everything for me... Natangaza Rasmi kuondoka Chadema na Kurudi Nyumbani....

Feels good to be Back...

Mapema mwaka huu (Februari), msanii huyo alihamia chama cha CHADEMA akidai ameenda kupigania demokrasi ambayo alidai ilikuwa inafifia nchini.

"Kuanzia sasa mimi siyo tena mwanachama wa CCM, na muda mfupi ujao nitachukua kadi yangu ya CHADEMA... Nimeamua kuingia CHADEMA kwa sababu nataka kupigania demokrasia, laiti ningejua, ningeingia zamani sana, najua nimewahi kusema kuwa nitakufa nikiwa CCM, lakini sikujua kama itakuwa hivi, laiti ningejua mapema basi nisingesema vile na ningejiunga CHADEMA muda mrefu sana, kwa sasa I am a proud member of CHADEMA" alinukuliwa Wema Sepetu mara baada ya kuhamia upinzani.

Aidha, msanii huyo anakabiliwa na shtaka la kutumia dawa za kulevya wakili wake akiwa ndg. Alberto Msando ambaye naye katimkia CCM toka ACT-Wazalendo.

Aidha, vipodozi vya msanii huyo (Kiss) vimepigwa marufuku na Serikali kuwa havifai kwa matumizi ya binadamu.
Share:

Search This Blog

  • ()
Powered by Blogger.

Yaliyojiri leo

Tanzania yaanza majaribio dawa kinga ya Ukimwi

LIKE OUR FACEBOOK PAGE

Contact us

Name

Email *

Message *